WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mipango na Uwekezaji), Profesa Kitila Mkumbo, amepongeza ubunifu ulioonyeshwa na wanafunzi wa Chuo cha St Joseph jijini Dar es Salaam, akisema ukiendelezwa unaweza kutatua changamoto nyingi zinazoikabili jamii.
Amesema Serikali itashirikiana na vyuo binafsi kuhakikisha masomo ya sayansi yanapewa kipaumbele ili kupatikane wahandisi wengi nchini na kuondoa utegemezi wa wataalamu wa kigeni. Aliyasema hayo mwishoni mwa wiki wakati akizungumza kwenye Wiki ya Tafiti na Ubunifu ya Chuo cha St Joseph, ambapo wanafunzi walionyesha ubunifu wa teknolojia mbalimbali za uhandisi.
Profesa Mkumbo alisema chuo hicho kwa muda mrefu kimekuwa mstari wa mbele kutoa wataalamu wa sayansi na kukitaka kuendelea kuchukua nafasi yake miongoni mwa vyuo vinavyotoa wataalamu wengi wa fani hiyo nchini. Alisema ametembelea maonesho ya kitaaluma ya wanafunzi na kubaini kuwa wamebuni vitu mbalimbali ambavyo vinaweza kuwa na manufaa kwa taifa.
References:
MICHUZI News